Home
About
Contact
Header Ads Widget
Home
News
Entertainment
Sports
Magazeti
Home
kitaifa
RUNALI YAGAWA MBEGU ZA UFUTA NA ALIZETI BURE KWA WANACHAMA WAKE
RUNALI YAGAWA MBEGU ZA UFUTA NA ALIZETI BURE KWA WANACHAMA WAKE
Misalaba
Tuesday, February 13, 2024
NA HADIJA OMARY
Ili kuongeza uzalishaji wa zao la Ufuta na kufanya uhamasijaji kwa wakulima kulima zao la Alizeti chama Kikuu cha ushirika RUNALI kinachohudumia wakulima wa Wilaya za Ruangwa Nachingwea na Liwale Mkoani kimegawa mbegu za mazao hayo bure kwa wakulima wanachama wake
Akizungumza wakati wa ugawaji wa Mbegu hizo leo February 13 uliofanyika katika ofisi za Chama hicho Wilayani Nachingwea Mkuu wa Wilaya ya hiyo Mohamed Moyo aliwataka viongozi wa vyama vya msingi AMCOS kwenda kuzigawa Mbegu hizo kwa wakulima waliokusudiwa sambamba na kuweka utaratibu rafiki katika ugawaji wa mbegu.
Hata hivyo moyo pia aliwasisitiza wakulima kuwatumia na kufuata maelekezo ya maafisa Ugani wakati wanapoenda kuandaa mashamba yao.
Meneja Mkuu wa chama hicho Jahida Hassan amesema mbegu hizo zimegawa ni tani 2 za ufuta na tani 4 za Alizeti na zimegaiwa kwa kuzingatia maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa ufuta, maeneo ambayo hayastawi mazao mbadala kwa alizeti pamoja na maeneo yaliyopata athari ya mvua na wanyama waalibifu kama tembo
"Kama mnovyojua mwaka huu mvua zimekuwa nyingi sana kuna maeneo kuna maeneo ambayo yameathiriwa na mvua wakulima walipanda Ufuta lakini umezolewa na mvua kwa hivyo tumezingatia pia hayo maeneo mfano kama namapwia, lionja hayo ni maeneo yaliyoathirika na mvua na tembo"
Kwa upande wake Afisa ushirika Mkoa wa Lindi projestus Paschal amewapongeza Runali kwa kutoabegu hizo kwa wanachama wake ambapo amesema itendo ni utekelezaji wa msingi wa saba wa ushirika ambao unawataka vyama pindi wanapokusanya tozo wahakikishe wanarudisha kwa jamii
Mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika RUNALI Odas Mpunga amesema hiyo ni mara ya pili kwa chama cha Chao kugawa mbegu kwa wakulima wao ambapo kwa sasa wameanza kuona tija baada ya msimu uliopita wa 2022/2023 ambapo uzalishaji ulikuwa tani elfu 16 lakini baada ya kugawa mbegu mwaka 2023/2024 uzalishaji ulipanda hadi kufikia hadi tani elfu 23 na sasa matarajio yao kuongeza mpaka kufikia tani elfu 30 kwa msimu ujao wa 2024/2025
Kwa upande wao wakulima akiwemo Shamsia Naluchonga na Kasim Lada walikishukuru chama chao kwa kuwapatia mbegu hizo bure ambapo walisema mbegu hizo zitawasaidia kuongeza uzalishaji katika mazao hayo
Post a Comment
0 Comments
MAGAZETI
NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI
TV News
World News
UZA NUNUA NASI LEO
Subscribe Us
MATANGAZO
TIBA YA UKANDAJI WA MGONGO, KICHWA KUTOKA NEEMA BEAUTY, SPA SALOON
MAKALA NZURI ZAIDI
WAKULIMA WA PAMBA IGUNGA WAPONGEZA BBT ILIVYOWAFIKIA MASHAMBANI.
BARIADI NEWS
Wednesday, May 14, 2025
Na COSTANTINE MATHIAS, Igunga. WAKULIMA wa Pamba kutoka vijiji vya Mbutu na Mwang'…
STAY CONNECTED WITH US
Ad Space
Responsive Advertisement
Most Popular
HAYA HAPA MAJIMBO MAPYA
Monday, May 12, 2025
NAFASI ZA KAZI NEC UCHAGUZI MKUU 2025
Friday, April 04, 2025
RAIS SAMIA ATOA MILIONI 50 KUCHANGIA UJENZI WA KANISA KIGOMA
Monday, May 12, 2025
Contact form
0 Comments