Header Ads Widget

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA WAFANYAKAZI TANESCO MKOA WA IRINGA WALIVYOKULA PAMOJA NA WATOTO WA KITUO CHA HURUMA CENTER


meneja wa Mkoa Afisa Rasilimali watu wa Mkoa Bi Frida  Barankena akimlisha mtoto wa kituo Cha Huruma Center 

Meneja wa Tanesco mkoa wa Iringa Dotto Chacha akizungumza na wafanyakazi wa Tanesco 






















































 TANESCO IRINGA YASOGEZA TABASAMU KENYE KITUO CHA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU CHA HURUMA CENTRE

27 Julai 2024

Na Juma Msuya

Uongozi wa TANESCO Mkoa wa Iringa ukiongozwa na Meneja wa Mkoa Mhandisi Dotto Chacha umesogeza tabasamu la kuendeleza furaha kwa jamii  ikiwa ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha mwaka mpya wa 2024, matukio yafuatayo yamefanyika siku hiyo:-

1:Kutoa zawadi ya vitu, vifaa na vyakula mbalambali

2:Kuweka umeme kwenye mita tatu za Mabweni ya kulala watoto ya Huruma Centre

3: Kufanya usafi maeneo mbalimbali ya Kituo

4: Kununua mahitaji, kupika na kushiriki chakula cha pamoja na watoto wenye mahitaji maalumu

5: Kutoa elimu ya huduma mbalimbali zilizolenga kujenga mahusiano mema ya watoto, wafanyakazi wa kituo na watumishi wa TANESCO.

📍 Tukio hilo limehusisha michango iliyochangwa na wafanyakazi wa TANESCO Mkoa  Iringa na wilaya zake

📍Akikabidhi zawadi hizo kwenye kituo kwa niaba ya meneja wa Mkoa Afisa Rasilimali watu wa Mkoa Bi Frida  Barankena alisisitiza kuwa kazi hii ya kurudisha kwa jamii ni endelevu ikiwemo kushiriki kwenye matukio mengine yanayohusu jamii haswa upandaji wa miti ili kuendelea kuboresha mazingira.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano na Huduma kwa wateja

Mkoa wa Iringa



































Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI