Header Ads Widget

KITABU CHA UFAHAMU WA KANISA HALISI CHAZINDULIWA NJOMBE

Mkuu wa wilaya ya Njombe Mhe.Kissa Kasongwa akizindua kitabu cha Ufahamu.

Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE 

Wakati jeshi la polisi likiendelea na doria kwa kutumia silaha kukabiliana na wahalifu nchini viongozi wa dini mkoani Njombe nao wametakiwa kuendelea na doria za kiroho kwa lengo la kuwarejesha kwenye mstaari wanaokiuka sheria za nchi.


Agizo hilo limetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe John Makuri Imori katika zoezi la uzinduzi wa kitabu cha ufahamu  wa kanisa halisi la mungu baba uliofanyika mkoani Hapa na kwamba viongozi wa dini wanapaswa kuendelea kuisaidia serikali kukabiliana na wahalifu kwa kueneza injili.


Akizindua kitabu hicho mgeni wa heshima Kissa Kasongwa mkuu wa wilaya ya Njombe amekiri kuwa kanisa Halisi limekuwa miongoni mwa makanisa yanayochochea amani katika wilaya na mkoa tofauti na makanisa mengine kwenye baadhi ya mataifa ambayo yamekuwa yakiripotiwa kujihusisha na makundi ya ugaidi.


Izrael Charles ni mtekelezaji wa amani halisi toka  kanisa Halisi la mungu baba mkoani Njombe ambaye anasema kitabu cha ufahamu kimebeba ujumbe katika mambo manne ikiwemo Ufahamu wa kumjua Mungu.


Kiongozi mkuu wa kanisa hilo Baba Halisi amesema hivi sasa wameendelea kueneza injili kwa kutumia lugha ya kiswahili katika mataifa ya Rwanda,Uganda,DR Congo,Msumbiji na Kenya ambako pia wamekubaliwa kutokana na kazi njema ya kuhamasisha amani ambayo inawasaidia viongozi wa serikali kuwaongoza vyema wananchi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI