Header Ads Widget

MBUNGE WA JIMBO LA MOSHI VIJIJINI ACHANGIA BAJETI YA WIZARA YA ELIMU VYUO VIKUU VYAPATIWA USHAURI KUJULIKANA KIMATAIFA



NA WILLIUM PAUL.

Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini Profesa Patrick Ndakidemi amechangia  hotuba ya bajeti ya Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia ambapo ameipongeza Wizara ya Elimu  na watendaji wote kwa ushiriki wao kufuta Ujinga, Maradhi na Umaskini.


Mbunge Ndakidemi alimshukuru Rais kwa uwekezaji mkubwa kwenye   Sekta ya elimu ambapo alijikita katika  ubora wa vyuo vikuu vya Tanzania ukilinganisha na vyuo vya Afrika na duniani kwa ujumla.

Mbunge alisema licha ya nchi yetu kuwa na miundombinu bora ya elimu, vyuo vikuu vya Tanzania havina nafasi nzuri barani Afrika ukilinganisha na Afrika Kusini, Kenya na Uganda.


Alisema kuwa viongozi  wetu wa vyuo vikuu wamekosa ubunifu kutangaza vyuo vyao pamoja na baadhi ya wasomi wa vyuo vyetu vya  Kitanzania kutochapisha tafiti zao kwenye majarida ya kimataifa.  

Alieleza athari za kufanya hayo ni nchi kukosa heshima ya kimataifa na Wahadhiri kupoteza umaarufu kwenye jukwaa la wasomi hali ambayo imechangia vyuo kukosa wadau wa Kimataifa kufanya nao kazi za kitafiti.


Mbunge alishauri Wizara ihakikishe Wahadhiri na  wanafunzi wote wanaosomea shahada ya pili na ya tatu wanajisajili kwenye google scholar, pamoja na Wahadhiri na watafiti wetu wachapishe kazi zao kwenye majarida ya  kimataifa, Vyuo vikuu viwe na sera ya kuweka machapisho, picha za matukio yote mtandaoni katika tovuti za vyuo.

Mwisho.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS