Header Ads Widget

WATU WATANO WAFA KWA AJALI YA MGODINI NA GARI IRINGA AKIWEMO MWANDISHI WA HABARI RASHID MSIGWA

 

Mwanshishi wa Habari Rashid Msigwa siku ya harusi yake 

WATU  watano  wamefariki dunia kwa ajali  mkoani  Iringa  akiwemo  mwandishi wa Habari Rashid Msigwa (38) mkazi  wa Igumbilo  mjini  Iringa  na  wengine  wanne  waliofariki  dunia  kwa  kufukiwa  na  kifusi katika  mgodi wa Grace  Chura  uliopo  Kijiji cha Igomaa kata ya   Sadani Wilaya ya  Mufindi  mkoani hapa.

Kamanda  wa  polisi  wa mkoa  wa  Iringa  Allan Bukumbi  aliwaeleza  wanahabari Leo ofisini  kwake   kuwa katika  tukio la kwanza  lililotokea  majira ya  saa 7 usiku   wa  kuamkia Leo  April  19,2023   mwandishi wa Habari Msigwa  akiwa na gari  binafsi aina  ya  Alteza Toyota Mazda yenye  namba  za  usajili T995 iliyokuwa  ikiendeshwa na marehemu  Msigwa .

Alisema  kuwa ajali  hiyo  ilitokea  eneo la  Ipogolo  Jirani na  Stendi ya  Ipogolo  katika  barabara  kuu ya  Iringa – Mbeya  kuwa   dereva wa  gari  hilo  alikuwa akijaribu  kumkwepa mwendesha  pikipiki na hivyo kugonga   pikipiki  hiyo iliyokuwa ikiendeshwa Joel Mgudula (23) makazi  wa Ipogolo  ambae  alijeruhiwa  mguu.

Alisema  kutokana na gari  hiyo  kuwa katika  mwendo mkali dereva wa gari alishindwa  kulimudu gari  hilo  na  hivyo  kupelekea  kugonga pikipiki kisha mti na kupelekea  kujeruhiwa  vibaya maeneo mbali mbali ya mwili  wake na wakati akikimbizwa  Hospitali kwa matibabu  alifariki  dunia .

 

Kwa  mujibu wa kamanda Bukumbi inasemekana   Msigwa  alikuwa katika  mwendo  mkali  na ndio chanzo cha ajali  hiyo  hivyo kutoa  wito kwa madereva  kuheshimu sheria  za usalama  barabara  na kuepuka  mwendo kasi .

Kwa  upande wa  shuhuda wa ajali  hiyo  Adam  Sanga  ambae ni dereva   boda boda  eneo hilo  alisema  kuwa  dalili  za  gari  hilo kupata ajali walizoana hata kabla ya  kumgonga mwendesha  boda boda  kwani  gari  ilikuwa  ikija mbele yao kwa mwendo mkali  na kjuwalazimu  boda boda  waliokuwepo  eneo hilo la  nje ya stendi la Ipogolo    kukimbia kukwepa  ajali ndipo  alipokwenda  kumgonga boda boda  mwenzao  aliyekuwa akijaribu  kuingia stendi ya Ipogolo .

Katika  tukio  la  pili  Kamanda  Bukumbi  alisema kuwa  zadi ya  watu  saba  walifukiwa na kifusi  katika mgodi  unaomilikiwa na  Grace  Chura  kwenye  Kijiji cha Igomaa kata ya  Sadani wilaya ya  Mufindi  ambapo  jitihada za kuwatoa  wahanga  hao  zilizaa matunda kwa  watu watatu  huku  wanne kati yao  wakipoteza Maisha .

Alisema kuwa  tukio  hilo limetokea  majira ya saa 2.30  usiku wa kuamkia Leo   April 19,2023  wakati  wachimbaji hao  wakiwa katika mgodi  huo .

 

Kamanda  Bukumbi  alisema  majira ya majeruhi  na  walipoteza Maisha  bado  kufahamika  kutokana  ugeni  wao  wa  wahusika katika  eneo hilo japo  jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi zai  ikiwa ni pamoja na kutafuta  mmiliki wa mgodi   huo  na afisa madini  ili  kujua kama mgodi   ulikuwa na kibali na taratibu  nyingine za uchimbaji .

Alitaja  chanzo cha  vifo vya wachimbaji hao  wadogo wa madilni  kuwa ni mvua kubwa  zinazoendelea  kunyesha na kupelekea ardh katika mgodi  huo  kuwa Nyevu nyevu ( Yenye maji maji)hivyo  kuporomoka. 


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI