Header Ads Widget

MAUAJI YA KUTISHA MAMA NA MTOTO WACHINJWA WAUAJI WATOWEKA NA KICHWA ,MIGUU NA MKONO



WATU  wasiojulikana   wamemuua kwa  kumchinja   kichwa na Kuondoka na  mkono ,mguu  poja na kichwa Cha mwanamke mkazi  wa  Kijiji cha Ilambilole wilaya ya Iringa mkoani hapa  Anitha Titus  Mbilinyi (48) na mwanae Andrea Mbwilo (7).
Akizungumza na Matukio DaimaTv shuhuda  wa  tukio  hilo  walisema  kuwa  tukio hilo  lilitokea  Februari 10 majira ya  jioni katika mpaka  wa  Kijiji  cha Ilambilole na Matembo wakati  mwanamke  huyo na mtoto  wake  wakitoka  shamba kufanya kazi  za kibarua  cha kupalia mahindi.
Elitha  Belo  ambae ni rafiki  wa marehemu  huyo  alisema kuwa kabla ya  taarifa ya  kifo  chake  alipata  kukutana na marehemu  na kuzungumza nae  na kumwahidi  kumlipa  deni lake la  shilingi 2000 alilokuwa  akimdai.
“ Nilikutana na marehemu Anitha  siku  mbili kabla ya kifo chake  na aliniomba  radhi kwa kuchelewa  kunilipa  deni langu la  shilingi 2000 na alisema  kuwa  jumapili  nitakuwa  nimepata  fedha  nitakulipa nikamwabia hakuna  shaka ila  nimesikitishwa  kupokea taarifa ya  kifo chake cha  kinyama”  alisema Elitha
Kuwa  siku ya Ijumaa jioni  ndipo  waliposikia  ngoma  ya Kijiji ikipigwa  kujulisha hali  wananchi  hali  isiyo ya kawaida  iliyotokea  kijijini hapo .
Alisema   baada ya  kufika ofisi ya  Kijiji  ndipo walipoelezwa  juu ya kutokea kwa  tukio la mauaji ya mwanamke  huyo na mwili  wake  kutelekezwa  kando la  barabara  ya lami kijijini hapo  umbali  wa Kilomita kama  moja  hivi  kufika  eneo la shule ya  Sekondari  Ilambilole.
Alisema  baada ya  kufika  eneo hilo  waliukuta  mwili  huo  ukiwa  hauna kichwa ,mguu mmoja na mkono mmoja baada ya  watu hao  waliotekeleza unyama  huo  kuondoka na viungo  hivyo .
 

Jane Titus Mbilinyi  Mdogo wa marehemu 
Akizungumza kwa niaba ya ndugu wa marehemu  huyo mdogo wa marehemu  Jane  Titusi Mbilinyi  alisema  kuwa  dadake  alikutwa na umauti majira ya saa 12  jioni wakati  akielejea  kutoka shambani  akiwa na mtoto wake Andrea  Emannuel  Mwilo aliyekuwa  akisoma  darasa la  pili  shule ya msingi Ilambilole
Alisema kuwa wauaji hao walipotekeleza mauaji hayo  walitoweka na baiskeli  ambayo alikuwa ameazima  kwa rafiki  yake aliyemtaja kwa  jina mmoja (jina  limehifadhiwa)ambaye  hadi  leo rafiki yake  huyo hajulikani alipo .
 
Hata  hivyo  alisema kabla ya  kifo  kumkuta  alipata  kuwasiliana nae kwa  njia ya  simu na akimsisitiza hali ya Maisha  ni ngumu na  kumtaka mdogo wake  huyo  kuendelea  kupambana na maisha .
“ Dadangu  baada ya  kuwasiliana kwa njia ya simu  alinisisitiza  kuwa  tuendelee  kupambana na Maisha ili  kulea  familia nay eye  aliniambia kuwa amepata kazi ya  kupalilia mahindi  shambani “
 
Alisema  kuwa mtoto Andrea  yeye  alimfuata mama yake  shambani baada ya kurejea   kutoka  shule majira ya saa 5  asubuhi ndipo  kifo  kilipomkuta huko.
 
Alisema kuwa  marehemu  alikuwa na Watoto  watano akiwemo Andrea aliyefariki na kati ya Watoto hao Watoto  watatu  wa baba mmoja na Watoto waliobaki  kila mmoja na baba yake na kuwa  baba  wa  Watoto  wote  walishafariki.
Mwenyekiti wa serikali ya kitongoji  cha Kihesa Kijiji cha Ilambilole  Angela Nyalusi  alisema  kuwa  taarifa ya  mauaji hayo  baada ya  kuipata  walitangaziana kila mwenyekiti wa  kitongoji  kufanya  upelelezi  wa kutambua  watu  wanaolimia mashamba  yao  eneo la Matembo  kutokana na mwili  wa  mwanamke  huyo  kutojulikana  kwa  kuwa  kichwa na nguo  walitoweka nazo wauaji hao .
“ Baada ya  kutangaziana  wenyeviti wote  ndipo  ilipobainika  kuwa  Anitha Mbwilo aliondoka  nyumbani  toka Ijumaa Kwenda  eneo  hilo la Matembo na hakurejea  ijumaa  hiyo hadi  usiku”
 
Alisema  wakati  wakitafuta  kichwa na viongo  walivyotoweka navyo  wauaji hao porini  ndipo  walipozikuta  nguo  za marehemu na  wakati  wakitafuta  zaidi  walikuta kichwa kikiwa  kimetupwa kwenye shimo la mchwa  na walipokitoa walikuta  na kichwa  cha mtoto wake na  viungo vingine  mguu na mkono japo  hadi  sasa kitovu cha marehemu bado  hawajakiona maana  waujaji hao  walikata chini ya tumbo na kuondoka na kitovu chake .
 
Mwenyekiti  huyo  alisema  kwenye  eneo lake  hakuwahi  kupata  taarifa  zozote mbaya  juu ya marehemu huyo wala  hakuna matukio  yoyote  ya ugomvi yaliyopata  kutokea yakimhusisha marehemu  huyo.
Huku  mwenyekiti wa  serikali ya Kijiji cha Ilambilole Jeiros Kiuno alisema  kuwa  tukio hilo  ni la kwanza  kutokea  katika  Kijiji   hicho na kuwa  hadi sasa  Kijiji  kinaendelea na msako  wa  kuwasaka  wahusika na mauwaji hayo .
“ Mimi taarifa ya mauaji haya nilipata  kutoka kwa mwanakijiji  mwenzetu  aliyekuwa  akitoka shamba japo  wakati  huo  wa siku ya ijumaa ilikuwa ni usiku ndipo tulikubaliana  utafutaji wa viungo  uanze  jumamosi  na  tulifanikiwa  kukuta  viungo na mwili wa mtoto wake”
 
Alisema  mwili  wa  mwanamke  huyo na mwanae alichukuliwa na  jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi na wanatarajia  kuzikwa leo  Kijiji cha Ilambilole  .
Kamanda  wa polisi wa  mkoa wa Iringa kamishna msaidizi wa  polisi (ACP) Allan Bukumbi alipotafuta kwa  njia ya simu ili kuthibitisha  tukio  hilo hakupatikana .
Mwenyekiti wa kamati ya  ulinzi na  usalama  wilaya ya Iringa ambae ni mkuu wa wilaya ya Iringa Veronica Kessy  alipotafutwa kwa njia ya simu  alisema  kuwa  yupo  safarini mkoani Mwanza  na  kumtaka mwandishi wa Habari  hizi  kuwasiliana na katibu tawala wa wilaya ya Iringa .
Kwa  upande wake katibu tawala wa  wilaya ya Iringa Stomen  Kyando  alithibitisha kutokea kwa maujaji hayo  na  kuwa taarifa  alizopata ni kuwa hadi sasa  watu wawili  wanashikiliwa na  jeshi la polisi  kwa  uchunguzi  zaidi .
Mganga mfawidhi  wa Hospitali ya  Rufaa ya mkoa  wa  Iringa Dkt  Alfred Mwakalebela alithibitisha kupokea  miili  ya marehemu hao.


Marehemu Anitha Titusi Mbilinyi enzi wa uhai wake
Mtoto Andrea Mbwilo enzi za uhai wake 
 
Eneo ambalo mauaji yalitokea
Shuhuda wa tukio 
Waombolezaji msibani 

Kijiji Cha Ilambilole

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI