Header Ads Widget

WAZIRI MASAUNI AAGIZA SHIMA KUTUMIA VEMA ARDHI YA GEREZA LA ISUPILO IRINGA

waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni akiwasili GEREZA la Isupilo Mufindi 
Maofisa magereza wakimpokea Waziri Masauni 


NA MATUKIODAIMAAPP, IRINGA 


WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni  amelitaka  Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza (SHIMA) kuhakikisha inatumia Ardhi ya Gereza la Isupilo wilayani Mufindi  mkoani Iringa kuongeza kasi ya uzalishaji  wa mazao ya chakula na biashara .
Akizungumza  jana  baada ya  ziara  yake  katika gereza la Isupilo waziri Mhandisi Masauni  alisema  kuwa mbali ya  kuanza kazi kwa  SHIMA ila amefarijika na mapokeo makubwa ya mabadiliko ndani ya  jeshi la magereza hasa katika mkoa wa Iringa  kutokana na jinsi  walivyopokea mabadiliko hayo mapya .

Hivyo  alisema  uwepo  wa SHIMA ni  fursa  kubwa kwa  magereza kutimiza  majukumu yao pia kunufaika  zaidi ya shirika   hilo kiuchumi kama  gereza na  wafungwa wanaomaliza muda  wao .

Alisema kuwa jambo kubwa shirika  ni  kusimamia shughuli za  kibiashara zitakazotokana na kilimo huku  magereza  wao  watafanya  shughuli  za  kusimamia  wafungwa  kwa  kuripoti  wa kamishana  wa  magereza Tanzania  huo  shirika  msimamizi  wake  atakuwa mkurugenzi mkuu wa  shirika .

Hivyo  alisema makubaliano kati ya shirika  na jeshi la magereza  kwa  wafungwa  yatakuwa ya  kibiashara  kati ya pande  hizo mbili na itasaidi magereza na wafungwa  kupata  faida ya nguvu  wanazotumia .

"  Sioni  ubaya  wowote  kwa  jeshi la magereza  kuwalipa wafungwa  watakaomaliza vifungo  vyao kwa  nguvu  watakayoitumia "

Novemba 3, 2022, ndipo waziri Mhandisi Masauni alipozindua   Bodi SHIMA ikiwa ni maono ya kibiashara na utekelezaji wa azma ya Rais DKt Samia Suluhu Hassan ambapo moja ya kipaumbele chake ni kuboresha Jeshi na mifumo yake.

Masauni alisema katika kutekeleza mipango hiyo, Rais aliongeza Bajeti ya jeshi hilo, ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ipasavyo kwa ufanisi na weledi.

Alisema kutoka na wajumbe wa bodi hiyo aliowateua kwa sifa na weledi wao, serikali ina matumaini makubwa kuwa watatekeleza majukumu yao kwa uzalendo wa kusaidia Taifa katika Jeshi la Magereza kusonga mbele zaidi.

"Ndugu wajumbe, lengo kuu la SHIMA ni kusaidia Jeshi la Magereza kutenganisha  majukumu ya kijeshi na biashara bila muingiliano wowote, ili kuwepo kwa mafanikio makubwa yakujiendesha na kuchangia pato la Taifa, hivyo ni matumaini yangu makubwa kuwa bodi hii itasaidia shirika hili kutimiza malengo hayo na kusonga mbele zaidi," alisema Masauni.  

Aidha, Waziri Masauni pia aliitaka Bodi hiyo aliyoizindua kutatua changamoto zilizopo, ambazo ni nikutokuwepo mfumo maalumu wa kujiendesha, kutozingatia kanuni na taratibu, kutokuwa na maono na nia ya dhati ya kujiendesha kibiashara na kutatua baadhi ya migogoro iliyopo.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI