Imekuwa rahisi zaidi Kwa klabu ya Ihefu FC kuigagadua Yanga 2-1 na kuvunja rekodi ya Yanga ya kutokufungwa katika mechi ya 50 kwenye mechi za ligi kuu Tanzania bara baada ya kufungwa kwa mabao 2-1, mchezo ambao ulipigwa Mbarali mkoani Mbeya.
Timu ya Yanga ilianza kupata bao kupitia kwa Yannick Bangala kabla ya Never Tigere kusawazisha kwa kupiga mpira wa adhabu uliomshinda kipa wa Yanga na kutinga nyavuni moja kwa moja.
0 Comments