Header Ads Widget

WAZIRI UMMY ATOA TAARIFA JUU YA MAPAMBANO YA UVIKO_19 KWA KIPINDI CHA MIAKA 2

 



Na Hamida Ramadhan Dodoma 


WAZIRI wa Afya Ummy mwalimu amesema hadi ufikia Machi 15 2022 jumla ya watu  elfu 33789 wamethibitika kuwa na virusi vya ugonjwa wa UVIKO 19 huku vifo vikiwa ni 803 kwa muda wa kipindi cha miaka miwili tangu kulipuka kwa ugonjwa huo hapa nchini


Ameyasema hayo leo jijini hapa wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO 19 kwa kipindi cha miaka miwili.


Waziri Ummy amesema idadi hiyo ni ndogo kwani serikali ilijikita kupima  watu ambao ni wagonjwa na wale wote waliokuwa wakisafiri tu na hawakuwa wakipima  kila mtu 


Pia amesema zaidi ya watu milioni 2  sawa na asilimia 9.17 ya watanzania wenye umri wa miaka 18 na kuendelea wamechanjwa chanjo kamili ya ugongwa wa UVIKO 19  huku akisema idadi hiyo ya uchanjai haridhishi  na kuwataka wakuu wa mikoa yote kuendelea kuwahamasisha wananchi kuchanja.


"Mikakati ya serikali ilijikita katika kuwatoa hofu wananchi kuhusu mlipuko huo kwa kufunga shule vyuo na taasisi za elimu za juu na utoaji wa elimu kwa jamii ya kujikinga kwa kukataza mikusanyiko isiyokuwa ya lazima kunawa mikono kutumia  vitakasa mikono kuimalisha huduma za ukaguzi kwa wasafiri wa badari viwanja vya ndege," amesema Waziri Ummy 


Aidha amesema kwa kipindi cha miaka miwili ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO 19 Tiba asili imeonekana imefanya vizuri kwani  imefanya kazi kubwa kwa kuwaondoa hofu wananchi na wannchi kuendelea kutumia.dwa za tiba asili.


 "Tiba asili ilituokoa kwa kiasi kikubwa kwa kipindi cha miaka miwili ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO  19 kwa kutuondolea mzigo katika sekta ya afya kwani ni ukweli kwamba sekta ya afya iko tete wagonjwa kibao miundombinu haitoshi watumishi wachache uhaba wa dawa na vifaa tiba hivyo  tuna kwenda kuboresha huduma za tiba asili,"amesema Ummy. 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI