NA HADIJA OMARY
Jumla ya Watoto wachanga 296 waliozaliwa Mkoani Lindi kwa kipindi cha Mwaka mmoja uliopita 2021 wamefariki Dunia kwa kukosa hewa .
Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Bi Rehema Madenge wakati wa ghafla fupi ya kupokea vifaa tiba kutoka taasisi ya Doris MOllel Fundationi iliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Lindi Sokoine.
Bi madenge alieleza kuwa swala la vifo kwa akina mama na Watoto wakati wa kijifungua bado ni changamoto katika Mkoa huo inayohitaji ufumbuzi kwani kwa mwaka 2021 kati ya akina mama 31109 waliojifungua watoto 30813 kati yao walizaliwa wakiwa hai huku Watoto 296 wakipoteza Maisha.
Alisema kuwa sababu kubwa iliyochangia Watoto hao kupoteza Maisha ni kukosa hewa kutokana na Watoto hao kuzaliwa kabla ya wakati ( Njiti).
Hata hivyo alieleza kuwa Mkoa huo kwa sasa una vituo 271 vya kutole huduma za Afya ambapo kati ya hivyo vituo 254 vinatoa huduma ya Mama Baba na Mtoto huku vituo 17 vikitoa huduma zingine za kawaida.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundationi, BI Doris Mollel akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo alieleza kuwa mashine hizo 9 za kufua hewa ya oxgeni zenye thamani ya milioni 35 zitagaiwa katika Halmashauri tau za Mkoa huo ambazo ni Mtama, Ruangwa pamoja na Mchinga huku akieleza wanufaika wa mashine hizo ni Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati hasa wale wanaopata changamoto ya upumuaji.
Kwa upande wake muuguzi kiongozi wodi ya Watoto wachanga Clementia Mlope katika hospitali hiyo ya sokoine amesema kwa mwezi wamekuwa wakipokea Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti) kati ya 20 hadi 25 kutoka vituo mbali mbali vya kutolea huduma ya afya ndani ya Mkoa ambapo ameeleza kuwa kupewa kwa vifaa tiba hivyo vinaenda kusaidia kwa kiasi kikubwa.
‘’Tunajua hawa Watoto wanazaliwa kabla ya siku zao kwa hivyo hata mapafu yao yanakuwa hayajakomaa hivyo wanahitaji msaada mkubwa sana wa kupumua kupitia hizi mashine kwahiyo kupatiwa kwa hizi mashine kutasaidia sanakuokoa Maisha ya hawa watoto’’.
Fatuma selemani ni mmoja kati ya akina mama waliojifungua kabla ya wakati aliupongeza uongozi wa Doris Mollel kwa kutoa vifaa hivyo vitakavyoweza kunusuru Maisha ya Watoto Njiti watakaozaliwa hospitalini hapo
0 Comments