Header Ads Widget

DC MUFINDI SAAD MTAMBULE AVUTIWA NA JITIHADA ZA MRADI WA YAM

Wanufaika wa mradi wa YAM

Ikiwa katika juhudi za kuwainua kiuchumi vijana na watu wenye mahitaji maalumu serikali kwa kushirikiana na wadau kutoka mradi  Youth Agency Mufindi (YAM)wameandaa mafunzo kwa vijana mbalimbali ili kuwasaidia kufikisha ndoto zao.

Wakizungumzia  kuhusu malengo yao baada ya kufika kwenye mafunzo hayo wanufaika hao wamesema wamejipanga vyema katika kuyapokea mafunzo kwani wanaamini ndoto zao za muda mrefu zitatimia lakini pia wataweza kumudu maisha yao pamoja na kuzikabili changamoto za maisha kwa ujumla.

Mwezeshaji wa mafunzo

Mwezeshaji wa mafunzo hayo Dkt. Heriel Mfangavo amesema mafunzo hayo yamejikita katika kuwasaidia vijana namna ya kujitegemea katika nyanja zote ili waweze kujikwamua katika changamoto wanazozipitia lakini pia kujiinua kiuchumi kwa kufanya shuguli mbalimbali za ujasiriamali 

Dkt Mfangavo ameongeza kuwa vijana ambao wanastahili kukaa kwenye makundi baada ya  mafunzo hayo wananufaika kwa kupata mikopo kutoka katika bajeti za halmashauri ambayo itawasaidia katika kuendeleza biashara zao lakini pia vijana ambao ni walemavu wanapewa kipaumbele cha kuweza kukopeshwa au kuingizwa kwenye fursa za ajira rasmi .

Meneja wa mradi YAM

Meneja wa mradi wa YAM Zilpa Mgeni wakati akitolea ufafanuzi kuhusu ushirikiano wa mradi na serikali amesema wanaishukuru serikali kwa kuonyesha ushirikiano wa hali ya juu na mradi wao ambao kiujumla una msaada mkubwa sana kwa vijana 

''Mimi na timu yangu tumeona huu mradi unasaidia kwasababu tumegundua kuwa kuna mbadaliko makubwa tangu tumeanza kuwabainikwani hapo mwanzo walikuwa hawajiaamini kwamba wanaweza kufanya biasharalakini baada ya kupata mafunzo ya saikolojia na ujasiriamali wao wenyewe wamekiri  kwamba wanaweza kufanya kitu ''. Amesema Zilpa

Pia ameongeza kwa kuiomba serikali kuzidi kutoa ushirikiano hasa kwa kusaidia kupatikana kwa mikopo hiyo ili wanufaika hao wapate mitaji na kuweza kujiendeleza kimaendeleo.



Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mufindi na diwani wa kata ya Luhunga Festo Elia Mgina amewataka vijana hao  kusikiliza vyema mafunzo hayo huku akiwaahidi kuwa pamoja na kuwahakikishia kupata mikopo baada ya mafunzo  yao kutokana na serikali kujipanga vyema katika kuwasaidia wahitaji.

Naye mkuu wa wilaya ya Mufindi Saad Mtambule wakati akifungua mafunzo hayo amewataka vijana hao kuzingatia masomo yao na kutokukatishwa tamaa na changamoto wanazokumbana nazo bali wajipe moyo na kuamini kuwa wakati wao wa kuinuka ni sasa hivyo hawana budi kukabiliana na changamoto hizo.

Mkuu wa wilaya ya Mufindi

Aidha amewasisitiza kutumia fursa hiyo ya mafunzo vizuri kwani serikali ya awamu ya sita ya rais samia suluhu hasan imejipanga vyema kuwainua na kuwasaidia wahitaji wote kutokana na kutenga fedha nyingi katika halmashauri zao hivyo wanachotakiwa kufanya ni kujitambua .

Pia ameongeza kuwa baada ya kupata mafunzo hayo jambo la msingi ni kuyatekeleza kwani utekelezaji wao utapunguza mazingira ya vitendo vya uhalifu na ukatili wa kijinsia katika jamii zao  huku akiwataka kuwatumia viongozi wao wakati wanapohitaji msaada .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI