MABIBTI waliopo kwenye Mradi wa Youth Agency Mufindi (YAM) ambao walikatisha ndoto za maisha baada ya kupata mimba za utotoni wameshukuru mradi huo kuwafikia na kuahidi kuja kuwa na mafanikio ya kiuchumi .
Wakizungumza na Matukio DaimaTv wakati wa mafunzo ya siku 10 yanayoendelea Ukumbi wa Yatima Igoda wilaya ya Mufindi Anles Msindila ,Debora Mdobofu na Adelina Hawa wamesema mbali ya ndoto zao kukatishwa na mimba Kwa Sasa wanajitambua na wamejipanga kuwa wajasiriamali Wazuri baada ya mafunzo hayo .
Pia mabinti hao wametoa Rai Kwa wenzao waliopo mashuleni kuzingatia masomo na kuachana na haraka ya maisha Kwa kupenda tabia za mahusiano ya kimapenzi wakiwa wadogo
Mradi wa YAM unatekelezwa kwenye vijiji 16 na kata tatu za Luhunga ,Mdabulo na Ihanu unaendeshwa Kwa ushirikiano na serikali ya Halmashauri ya Mufindi mradi ambao kiujumla una msaada mkubwa kwa vijana na ni miaka minne toka mwaka 2021/2024 umefadhiliwa na serikali ya Finland chini ya taasisi yake ya Diaconess kwa ushirikiano wa serikali ya Tanzania chini ya Halmashauri ya wilaya ya Mufindi na taasisi ya Foxes Community and Wild Life Conservation.(FCWC)
0 Comments