MJI wa Iringa Leo umekubwa na taharuki kubwa baada ya tukio la moto kutokea katika benk ya NMB tawi la Mkwawa huku kamanda wa polisi mkoa wa Iringa wa Iringa Allan Bukumbi akisema kwenye tukio hilo wafanyakazi watatu wa benki hiyo wamejeruhiwa na kukimbizwa katika Haspitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa .
Baadhi ya wateja wa benki hiyo waliokuwepo wakati moto huo ukianza kuwaka walisema walipatwa na mshituko mkubwa baada ya kutokea kwa tukio hilo huku magari ya zimamoto na uokoaji yakiwa nje ya jengo hilo na kuanza kupambana kuzima moto huo .
Alisema mteja Godlove Yona kuwa akiwa katika foleni ya kuhudumiwa alisikia wafanyakazi wa benki hiyo wakiwataka wateja kukimbia nje ya jengo kwani hali ya hatari imejitokeza kwa moto kuanza kuwa ndani ya jengo hilo .
Akizungumza na waandishi wa habari juu ya tukio hilo kamanda Bukumbi alisema kuwa kutokana na tukio hilo ni watu watatu wamejeruhiwa na kuwa kuhusu suala la usalama wa mali za benki hiyo hadi sasa hakuna upotevu wa fedha zaidi ya kuwepo kwa uharibifu kiasi katika chumba cha mkutano ambako moto huo ulianzia.
Kamanda Bukumbi mbali ya askari wa jeshi la polisi kufika kwa wakati eneo hilo pia amewapongeza wafanyakazi wa benki ya NMB tawi la Mkwawa ,jeshi la zimamoto na uokoaji kwa kufika kwa wakati eneo hilo kusaidia kuthibiti moto huo .
Aidha aliwataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari hasa yanapotokea matukio ya hatari kama ya moto na mengine kuacha kukimbilia sehemu ya tukio kwani ni hatari kwa usalama wao.
Meneja wa Benki ya NMB Iringa Colman Kiwia alisema kuwa tukio hilo la moto lilikuwa ni zoezi la utayari wa majanga ya moto kwa mujibu wa sheria ya usalama kazini inayowataka kufanya hivyo na benki hiyo kwa mujibu wa sheria ya usalama maeneo ya kazi na kuwa tukio hilo si halisi kwani limefanywa kama sehemu ya kutimiza matakwa ya kisheria ya sheria za usalama sehemu za kazi .
" Niwaambie tu majanga ya moto hayaepukiki lakini tunaweza kuchukua tahadhari ya majanga haya ya moto kwa kukata bima za majanga kuepuka hasara ambapo benki ya NMB tumekuwa tukitoa huduma ya bima hiyo na nyingine kama magari ,vifo na elimu bima zote zinatolewa pamoja na mambo mengine tunatoa mikopo ya kilimo , biashara na tuna ofa maalumu ya Uwekezaji Amana kwenye akaunti ya JASIRI bundi inayoishia tarehe 21 Machi "
Kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa Isabela Mbwago alisema kuwa wananchi wanapaswa kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo kwa kupiga namba 114 pindi yanapotokea majanga ya moto japo alitoa angalizo ya matumizi sahihi ya namba hiyo .
0 Comments