NA MWANDISHI MAALUM, NEW YORK, MAREKANI
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro amewataka Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani kuweka nguvu za kutosha katika kufanya Diplomasia ya Uchumi ikiwemo kuwavutia watalii kutoka nje ya nchi kuja nchini.
Ametoa kauli hiyo leo wakati mara baada ya kufanya ziara ya kutembelea ofisi ya Ubalozi huo ikiwa ni muendelezo wa kuzungumza na Watumishi na Wawekezaji mara baada ya kumalizika kufanyika kwa mkutano wa 50 wa mwaka wa uwindaji wa kitalii uliofanyika katika Jiji la Las Vegas nchini Mareakani.
Akizungumza na timu ya Watumishi hao, Dkt. Ndumbaro amempongeza Balozi wa Tanzania Nchini Marekani, Dkt. Elsie Kanza kwa kazi kubwa anayoifanya ya Diplomasia katika tasni ya biashara na utalii.
Ambapo amewataka Wanadiplomasia hao kuwa daraja katika kuwawezesha watalii kuja nchini Tanzania
Amesema Diplomasia ya uchumi katika tasnia ya utalii, Wanadiplomasia hao wanapaswa kutangaza na kujibu maswali ya watu mbalimbali wanaotaka kutalii Tanzania kuhusu namna ya kufika nchini kiujumla na katika kila kivutio cha utalii kimahususi.
"Kutokana na kasi kubwa ya maendeleo ya kiuchumi, Wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi Diplomasia ya kiuchumi ndo injini ya maendeleo haikwepi, ongezeni ujuzi katika eneo hilo." amesisitiza Dkt. Ndumbaro.
Aidha, Dkt. Ndumbaro amewahimiza Watumishi hao kuwa mstari wa mbele katika kujua masuala ya uwekezaji na biashara pamoja na mambo yote muhimu kuhusu utalii nchini ili waweze kuwaelezea wananchi wanaowahudumia
Vilevile amewataka kusababisha watalii kutoka katika nchi waliyopo kuhudhuria katika mikutano, makongamano na maonyesho ya utalii ya ndani ya Tanzania ikiwemo
matamasha ya kiutamaduni .
Katika hatua nyingine, Dkt. Ndumbaro amempongeza na kumwalika nchini Tanzania, Kiongozi wa Vyama vya Waongoza Watalii nchini Marekani, Rumit Mehta kuja kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko Ukanda wa Kusini.
0 Comments