Header Ads Widget

WAHAMIAJI HARAMU 40 WAKAMATWA IRINGA

 


Idara ya uhamiaji mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na vyombo vya usalama siku ya jumatano tarehe 12, 2022 majira ya saa 11 jioni imefanikiwa kuwakata wahamiaji haramu wapatao 40 raia wa Ethiopia.Mwandishi  Zacharia Nyamoga,Matukio Daima Iringa 

Akizungumza na waandishi wa habari Afisa uhamiaji Mkoa wa Iringa Agnes Luziga amesema wahamiaji hao walikamatwa katika gari aina ya fuso yenye usajili namba T-517 DJY mali ya Deogratius Kimambo raia wa Kilimanjaro likiwa limetelekezwa barabara ya Iringa – Mbeya

Akifafanua zaidi Agnes Luziga amesema baada ya upekuzi walifanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu wapatao 40 wakitokea Ethiopia kuelekea Afrika ya Kusini.

Aidha Agnes Luziga amesema wanaendelea na taratibu za kimahakama na watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani leo januari 13, 2022


Ameongeza kwa kutoa lai kwa Watanzania kutoa ushirikiano na vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo karibu  kwa kufichua pale wanapo waona watu ambao wanawatilia mashaka.

“Tunashirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kuwafichuwa hawa waharifu tunashirikiana kwa kupashana habari kama kuna matukio kama haya ili waletwe katika sehemu husika pia huwa tunatoa elimu katika redio kwa wananchi kuwa wanapo waona watu wanao watilia mashaka basi watoe taarifa ofisi au kwenye chombo chochote cha ulinzi na  usalama kilichopo karibu” Amesema Agnes Luziga

Kwa upande mwingine kamanda wa polisi mkoa wa Iringa ACP - Allan Bukumbi  akijibu kuhusu usalama mkoa wa Iringa kamanda amesema wahamiaji hao hawajahatarisha hali ya usalama kwasababu walikuwa wakipita tu kutoka Ethiopia kwenda Afrika ya kusini.

Pia ACP-Allan Bukumbi ameongeza kuwa wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa ujangili wakiwa na pembe za ndovu zenye zenye uzito wa kilogram 66.5 zenye thamani ya zaidi milioni mia mbili za Kitanzania.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI