Na WAF, Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe amewafunda Wakurugenzi wa Hospitali na taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo ikiwemo suala la kuwaendeleza Wataalamu wake.
Dkt. Shekalaghe amebainisha hayo mapema leo Januari 28,2022, wakati akiwasilisha mada katika kikao kazi kwa Wakurugenzi hao ambapo amesisitiza kuwaandaa mapema kwa kuwaendeleza wataalamu wa afya kwani itasaidia zinapokuja mashine mpya na za kisasa ziweze kutumika kwa ufanisi.
Kikao kazi hicho cha siku mbili, Wakurugenzi hao pia walipata kuwasilisha mada na majadiriano mbalimbali.
0 Comments