Header Ads Widget

POLISI IRINGA:TUMEKAMATA VIJANA WA PANYA ROAD 20 TUNAMSAKA KIONGOZI WAO KWA KOSA LA KUMFANYIA FUJO MKAGUZI WA POLISI

 

            RPC Iringa Juma Bwire

JESHI la polisi  mkoani  Iringa  limefanikiwa  kuwakamata   vijana  20   na  kuendelea  kumsaka  kiongozi wa  vijana  hao wanaofanya kazi ya  kuendesha  pikipiki (boda boda) maarufu  kwa jina la  Panya Road  ambao  wanatuhumiwa  kwa  makosa mbali mbali  yakiwemo ya  kiuhalifu na  kumfanyia  fujo   mkaguzi  wa  jeshi la Polisi Insepekta  Said  Tolage akiwa kazini .


kamanda  wa  polisi  wa  mkoa wa  Iringa Juma Bwire  aliwaeleza waandishi wa habari leo  ofisini kwake   kuwa   jeshi  hilo  limeendelea na oparesheni  mbali mbali  kwa  lengo la kuzuia na kuondoa uhalifu .

Alisema   katika  oparesheni   iliyofanyika   toka   Oct  8 mwaka huu  majira ya   4  asubuhi hadi saa 11  jioni  katika maeneo mbali mbali  ya  manispaa ya  Iringa  polisi  walifanikiwa  kuwakamata vijana  hao 20  wanaojiita  Panya   Road  ambao  wote  wakituhumiwa kwa kosa la  kufanya  fujo kwa  mkaguzi  wa polisi  na  askari wa  vyeo mbali mbali .

"  Askari  hao kwa pamoja   walishambuliwa   vijana  hao wa panya Road  wakati   vijana  hao  wakijaribu  kuziondosha  pikipiki  zilizikuwa  zimekamatwa  kwa makosa  ya usalama barabarani  siku ya tarehe 8 huko maeneo ya  Kisima cha bibi mlima wa Ipogolo  askari  walikuwa  kazini  wakitekeleza majukumu yao kwa mujibu wa  sheria  "

Alisema  kati ya  watuhumiwa  wanaosakwa  yupo  mmoja  ambae ni  kiongozi wao  ambae  nyumbani kwake  kumekutwa vitu mbali mbali  vya  kiuhalifu pamoja na bangi  za kutosha .

Kamanda  Bwire  alisema  watuhumiwa  wote  wapo mahabusu  na msako mkali  unaendelea kufanyika  kuwasaka  washiriki  wengine  ambao walifanikiwa kutoweka na pindi watakapo kamatwa  watafikishwa mahakamani .





Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI