Header Ads Widget

AJALI YA BASI LA ISAMILO TUNAFUATILIA KUJUA UKWELI -DC MOYO

Kufuatia taarifa zilizozagaa mitandaoni kuhusu kutokea kwa tukio la ajali katika eneo la Izazi wilaya ya Iringa katika barabara kuu ya Iringa -Dodoma haiku huu ,mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Moyo  ambae ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya amesema wanafuatilia taarifa hizo ili kupata ukweli .

Moyo amesema hayo usiku huu alipozungumza na Matukio Daima media kwa njia ya simu ,alisema tayari ofisi yake na jeshi la polisi wanafuatilia undani wa taarifa hizo kwa kwenda eneo la tukio .


Huu ni ujumbe unaosambaa kwa kasi kwenye makundi ya WhatsApp  usiku huu .

"Habarini za wakati huu...Jamani kama mna ndugu,jamaa na Marafiki waliokuwa wanasafiri leo na Basi la Kampuni ya ISAMILO linalofanya safari zake toka Mwanza kuelekea  Mbeya.Basi hilo la ISAMILO limepata ajalj hapa maeneo ya kijiji cha Izazi mkoani Iringa majira ya usiku huu.....Fanyeni Mawasiliano na wapendwa wenu ili kujua hali zao maana kuna waliojeruhiwa na kupoteza maisha pia ktk ajali hiyo.... *TUSAMBAZE TAARIFA HII KTK GROUP ZETU ZOTE*🙏🏽🙏🏽"

Matukio Daima tunaendelea kufuatilia undani wa taarifa hizi kupitia jeshi la polisi na ofisi zenye mamlaka ya kutoa taarifa  ili kujua undani wake .

Endelea  kuwa nasi .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI