Header Ads Widget

WHATSAPP YAFUNGA AKAUNTI KARIBU MILIONI 7 ZINAZOHUSISHWA NA SHUGHULI ZA ULAGHAI

 

Kampuni ya Meta inayomiliki WhatsApp, imesema imefunga akaunti milioni 6.8 zilizohusishwa na miradi ya ulaghai inayolenga watu kote ulimwenguni katika nusu ya kwanza ya mwaka huu.

Nyingi za akaunti hizi zimehusishwa na vituo vya ulaghai vinavyoendeshwa na mashirika ya uhalifu Kusini Mashariki mwa Asia, ambayo mara nyingi hutumia kazi ya kulazimishwa kutekeleza shughuli zao, kulingana na Meta.

Kampuni hiyo ilitangaza kufungwa kwa akaunti hizo, huku WhatsApp ikizindua hatua mpya za kukabiliana na ulaghai kwa kuwatahadharisha watumiaji kuhusu shughuli zinazoweza kutokea za ulaghai, kama vile mtumiaji kuongezwa kwenye gumzo la kikundi na mtu ambaye hayuko kwenye orodha yake ya mawasiliano.

Ulaghai ni mbinu ya kawaida ambapo wahalifu huingilia akaunti za WhatsApp au kuongeza watumiaji kwenye gumzo la vikundi ili kukuza miradi ya uwekezaji bandia na ulaghai mwingine.

Katika kisa kimoja kama hicho, WhatsApp ilifanya kazi na Meta na OpenAI, waanzilishi wa ChatGPT, ili kutatiza ulaghai unaohusishwa na kikundi cha wahalifu cha Cambodia ambacho kilikuwa kikitoa motisha za kifedha kwa kupenda (like) kwenye machapisho ya mitandao ya kijamii yanayokuza mpango wa kukodisha pikipiki ghushi.

Kampuni hiyo ilisema kuwa walaghai walitumia ChatGPT kutoa maagizo yaliyoelekezwa kwa waathiriwa watarajiwa.

Meta ilieleza kuwa walaghai mara ya kwanza huwasiliana na walengwa kupitia ujumbe wa maandishi, kabla ya kuhamishia mazungumzo kwenye mitandao ya kijamii au programu za kutuma ujumbe za kibinafsi, na kuongeza kuwa nyingi ya ulaghai huu ulifanyika kwenye malipo au majukwaa ya pesa taslimu.

Kampuni hiyo ilibainisha, "Daima mlaghai, na inapaswa kutumika kama ishara ya onyo kwa kila mtu: unapaswa kulipa mapema ili kupata mapato au faida iliyoahidiwa."

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI