Header Ads Widget

ZAIDI YA WATU 60,000 WALIUAWA GAZA KWA SHAMBULIO LA ISRAEL- HAMAS

 

Zaidi ya watu 60,000 wameuawa kutokana na kampeni ya kijeshi ya Israel huko Gaza tangu Oktoba 2023, wizara ya afya inayoendeshwa na Hamas inasema.

Ilisema Jumatatu idadi ya vifo ilifikia takribani 60,034, pamoja na watoto 18,592 na wanawake 9,782.

Takribani watu 112 waliuawa katika muda wa saa 24 kabla ya Jumanne asubuhi, na watu 22 waliuawa walipokuwa wakijaribu kupata msaada, wizara hiyo ilisema.

Wanawake na watoto ni miongoni mwa waliouawa katika mashambulizi ya usiku na asubuhi dhidi ya nyumba, vyanzo vya hospitali na mashuhuda waliiambia BBC.

Israel ilianza mashambulizi yake kujibu mashambulizi yaliyoongozwa na Hamas kusini mwa Israel tarehe 7 Oktoba 2023, ambapo takribani watu 1,200 waliuawa na wengine 251 kuchukuliwa mateka.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI