Header Ads Widget

UJENZI WA BARABARA YA LAMI KM 5.1 MKIMBIZI -MTWIVILA WAFIKIA PATAMU - ELIUD MVELLA

 


NA  CECILIA  PIUS MATUKIO  DAIMA  MEDIA

ALIYEKUWA  diwani  wa  kata ya   Mkimbizi  Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa  Eliud  Mvella  amesema  mchakato  wa  ujenzi  wa  barabara  ya  lami  kilomita  5.1 itakayounganisha  kata ya  Mkimbizi na Mtwivila  umefikia  hatua  nzuri na  tayari  mkandarasi  amekwisha   wasili  kukabidhiwa  eneo  la kuanza  ujenzi  huo .

Kuwa  ujenzi   huo  utatoa fursa  kuwa kwa  wananchi wa  kata   ya  Mkimbizi na Mtwivila  ambao  wanasifa  ya  kufanya kazi  mbali mbali katika  mradi huo  pia  wale  wenye  biashara  mbali mbali kwani wafanyakazi wa  mradi huo  watahitaji  huduma  kutoka kwao.


Akizungumza   katika  kipindi  cha Tanzania  ya  Leo kilichorushwa na  Matukio  Daima  Tv  Mvella  alisema  kuwa  ujenzi  wa barabara  hiyo ni matokeo  mazuri ya kazi  zinazofanywa na  serikali ya  awamu ya  sita  chini ya  Rais  Dkt  Samia  Suluhu  Hassan   na  wao katika  wasaidizi  wake ngazi ya kata  ya  aliyekuwa  mbunge  wa  jimbo   hilo Jesca  Msambatavangu  kuwa msimamizi  ngazi ya  jimbo miradi  hiyo  imekuwa kielelezo  kizuri .

"  Tunamshukuru  Sana  mheshimiwa  Rais  Dkt  Samia  Suluhu  Hassan  kwa  kazi nzuri  kwani  ujenzi  wa barabara  hii utakuwa  mkombozi  mkubwa  wa  maendeleo na  uchumi  wa  wananchi  wa kata ya Mkimbizi  pia  Manispaa ya Iringa  ambao  watanufaika na  barabara  hiyo " 

Alisema  kuwa barabara ya  Mkimbizi -Mtwivila  imekuwa  kero  kubwa  kwa  wananchi na  watumiaji wa  barabara  hiyo kutokana na  ubovu  uliokithiri  hasa  wakati wa masika  kutokana na barabara  hiyo  kutopitika kwa urahisi .

Hivyo alisema  hatua ya  ujenzi  huo  kuanza  utasaidia  kuondokana na changamoto   hiyo ya  ubovu  wa miundo  mbinu  kwani  ujenzi  huo utachagiza   ukuaji wa uchumi kwa  wananchi  wa eneo hilo.

Mvella  alisema  tayari mkataba wa  ujenzi wa barabara  hiyo  umekwisha  sainiwa toka  Juni 25 na mkandarasi  amefika  kuoneshwa  eneo la  mradi  toka Julai 15 mwaka  huu  na  kuwa  wakati  wowote  kazi itaanza  baada ya mkandarasi  huyo kulipwa fedha anzio za  kazi  hiyo .

Hata  hivyo  aliwataka  wananchi  wa Mkimbizi  kuendelea  kuwa na  matumaini na  serikali  ya  chama  cha mapinduzi  (CCM) kwani  ipo  kwa  ajili ya  kuwatumikia  na  kutatua  changamoto  mbali mbali  kama  ilivyofanya katika  sekta ya  elimu na  afya .






Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI