Na chausiku said
Matukio Daima, Mwanza
Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta, ataongoza kikosi cha mastaa zaidi ya 18 kutoka klabu kongwe nchini Simba, Yanga na timu nyingine za Ligi Kuu katika tamasha la Alliance Day litakalofanyika Julai 9 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyamagana, jijini Mwanza.
Tamasha hilo limeandaliwa na Kitivo cha Michezo cha Alliance kwa lengo la kuenzi maisha ya aliyekuwa mwasisi wa kitivo hicho, marehemu James Bwire, sambamba na kusherehekea Jubilee ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa shule hizo za michezo.
Mchezo huo unatarajiwa kuanza saa 10 jioni, ukitanguliwa na matukio mbalimbali ikiwemo mbio za hisani zitakazowashirikisha wafanyakazi wa kituo, wadau wa michezo na mechi za watoto kutoka vituo vya kukuza vipaji vya soka jijini Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Kituo cha Alliance, Stephano Nyaitati, alisema zaidi ya wachezaji 18 wamethibitisha kushiriki tamasha hilo. Miongoni mwao ni nyota wa Yanga kama Prince Dube, Israel Mwenda, Djigui Diarra, Maxi Nzengeli, Salum Abubakar 'Sure Boy' na Jonas Mkude.
0 Comments