Header Ads Widget

BOTI ILIYOBEBA SHEHENA YA MIRUNGI KUTOKA KENYA YANASWA NA POLISI TANGA


Na Ashrack Miraji Matukio Daima 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga limetekeleza operesheni ya mafanikio usiku wa tarehe 22 Julai 2025 kwa kukamata boti aina ya fibre, rangi nyeupe, iliyokuwa ikisafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi kutoka nchini Kenya kupitia Bahari ya Hindi.

Akithibitisha tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi, amesema kuwa boti hiyo ilikamatwa na Kikosi cha Polisi Wanamaji (Marine) katika eneo la Mawe Mawili, Kijiji cha Kwale, mpakani mwa Wilaya ya Mkinga na Jiji la Tanga, kufuatia taarifa za kiupelelezi na ufuatiliaji wa kina wa mbinu zinazotumiwa na wasafirishaji haramu.

Kwa mujibu wa Kamanda Mchunguzi, watuhumiwa wawili waliokuwa kwenye boti walifanikiwa kutoroka baada ya kufika karibu na fukwe, lakini boti pamoja na shehena ya mirungi vilikamatwa.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga limeeleza kuwa litaendelea kuimarisha doria na operesheni maalum hususan katika maeneo ya baharini ambayo yamekuwa yakitumiwa na wahalifu kuvusha bidhaa haramu kutoka nchi jirani.

Aidha, Kamanda Mchunguzi ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa mapema kuhusu viashiria vyovyote vya uhalifu katika jamii, hususan vinavyohusiana na usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya.



 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI