Header Ads Widget

URUSI IMEKUSANYA WANAJESHI ZAIDI YA 100,000 KARIBU NA MJI WA KIMKAKATI WA UKRAINE, KYIV INASEMA

Urusi imekusanya wanajeshi 110,000 katika eneo la Pokrovsk kama sehemu ya juhudi zake za kuutwaa mji huo wa kimkakati wa mashariki mwa Ukraine, mkuu wa jeshi la Ukraine alisema Ijumaa.

Oleksandr Syrskyi amesema kwamba eneo karibu na Pokrovsk pamekuwa "mahali pa moto zaidi" kwenye mstari wa mbele wa kilomita 1,200 (maili 745) ambao unapitia mashariki.

Vikosi vya Urusi vimekuwa vikijaribu kukamata Pokrovsk kwa karibu mwaka mmoja , na kushambulia moja baada ya nyingine. Lakini licha ya kuwa na faida ya wazi katika suala la idadi ya wanajeshi na silaha zilizopo, Moscow imeshindwa kuutwaa mji huo.

Pokrovsk ni lengo la kimkakati la Moscow. Rais wa Urusi Vladimir Putin ameweka wazi kuwa lengo lake ni kuteka maeneo yote ya mashariki mwa Ukraine ya Donetsk na Luhansk vikosi vyake vinakalia kwa sehemu.

Kyiv na washirika wake wanamshutumu Rais wa Urusi Vladimir Putin kwa kukwama katika juhudi za kutafuta amani ili vikosi vyake viweze kuteka maeneo zaidi ya Ukraine.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI