Header Ads Widget

WALIMU LINDI WAKUMBUSHWA KUWEKA AKIBA

 



Mkurugenzi wa  manispaa ya Lindi  Mkoani Lindi Juma Mnwele   amewahimiza Walimu wa manispaa hiyo  kujenga tabia ya kujiwekea akiba  ya kiasi cha pesa wanazozipata pamoja na kupangilia vzuri matumizi yao ili waweze kufanya mambo ya kimaendeleo .



Mnwele ametoa Rai hiyo alipokuwa anazungumza na walimu wa shule za msingi na sekondari kutoka halmashauri ya manispaa ya Lindi na Mtama Katika warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Benk ya NMB.


Amesema ili waweze kuwa na Maendeleo swala la nidhamu ya pesa ni jambo la kipaumbele hivyo ni muhimu kutumia Mafunzo waliyoyapata Katika kupanua uwezo wao wa  kiuchumi sambamba na kupanga maisha Yao.


Faraja Ngongo ni meneja wa NMB kanda ya Kusini Amesema Program hiyo ya mwalimu spesho imelenga Kutoa Masuluishi mbalimbali ya kibenki na utunzaji wa fedha pamoja na kuongeza fursa kwa Walimu ambao wamekuwa ni Wadau wao wakubwa. 


Baadhi ya Walimu walioshiliki Katika warsha hiyo wakaeleza manufaa wanayoyapata kutokana na kifurushi hiko.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI