Header Ads Widget

AJALI YAUA WATOTO WAWILI WA FAMILIA MOJA.

Watoto wawili wa familia moja wamepoteza maisha papo hapo kwenye ajali iliyohusisha magari matatu iliyotokea leo Jumatano Novemba 9, 2022 katika mteremko wa Iwambi mkoani Mbeya.

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Benjamin Kuzaga amethibitisha kutokea ajali hiyo.

 

Kuzaga amesema ajali hiyo imetokea majira ya saa 12:45 basi aina ya Fuso namba T 601 DHC liligonga gari namba T 452 DHD Toyota Raum na kugonga magari mengine huku chanzo cha ajali hiyo kikitajwa kuwa ni mwendokasi wa gari hilo.

 

"Katika ajali hiyo ni watoto wawili wa familia moja (waliokuwa katika gari dogo) wamepoteza maisha, niendelee kuwaomba madereva kuwa waangalifu wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto ili kuondokana na ajali hizi," amesema Kuzaga.

 

Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wamesema tukio hilo lilitokea saa 12 asubuhi ambapo dereva wa gari aina Fuso alijitahidi kumudu gari lake lakini alishindwa baada ya kugongana ubavu na gari dogo.

 

Taarifa Zaidi juu Habari hii utaipata kupitia Hotnews ya Matukio Daima Tv ifikapo saa 12:00 Jioni.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI