Mahakama ya kimataifa ya makosa ya uhalifu, ICC inatarajia hii leo
kutoa maamuzi kuhusu ombi la dharura la Ukraine la kutaka Urusi isitishe
mara moja uvamizi wake, huku serikali ya mjini Kyiv ikidai kuwa Urusi
ilimtuhumu kwa uongo jirani yake huyo anayeunga mkono nchi za Magharibi
kwa mauaji ya halaiki ili kuhalalisha vita hivyo. Hata hivyo Urusi kwa
upande wake ilidai kuhalalisha matumizi ya nguvu dhidi ya Ukraine kwa
lengo la kujilinda. Hukumu hiyo itatolewa mjini The Hague baada ya
Ukraine kuwasilisha ombi hilo la dharura muda mfupi baada ya shambulizi
la Urusi la Februari 24. Kyiv inaitaka mahakama hiyo kuchukua hatua za
muda mfupi kwa kuiagiza Urusi kusimamisha operesheni zake mara moja
wakati idadi ya wakimbizi kutoka Ukraine wakipindukia milioni 3 huku
majeshi ya Urusi yakizidisha mashambulizi kwenye majengo ya makazi mjini
Kyiv.
0 Comments