WANUFAIKA wa shirikisho la mageuzi ya kijani Afrika(AGRA) mkoani Iringa wamemweleza mjumbe wa kamati ya mipango bodi ya AGRA Dkt Jakaya Kikwete ambae ni Rais wa awamu ya nne wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania changamoto wanazokabiliwa nazo katika kukuza mitaji yao .
Akizungumza jana mjini Iringa wakati wa ziara ya mjumbe huyo wa bodi ya AGRA na msafara wake ,Mnufaika Emanuel Sanga ambae ni msambazaji wa Pembejeo kutoka kampuni ya Iwawa General Supplies mbali ya kupongeza AGRA kwa kuwaunganisha na wanavikundi wapatao 20 vijijini na sasa wamekuwa wakienda vizuri pamoja na uwepo wa changamoto ambazo wameomba serikali kupitia wizara ya Kilimo kushughulikia .
Alisema kupitia jitihada hizo za AGRA kuwaunganisha na vikundi vya wajasiriamali wadogo vijijini na elimu mbali mbali ambazo wameendelea kuzitoa bado wanaomba wizara ya Kilimo kuangalia uwezekano wa kuwainua zaidi kwa kuwapatia mikopo ya kukuza biashara yao.
“ Kupitia mafunzo yaliyotolewa na AGRA kwa wakulima na wasambazaji wa Pembejeo imesaidia wao kuongeza mitaji yao kupitia mkopo wa taasisi ya kibenk ambao waliomba ili kukuza biashara hiyo”
Alisema changamoto ni mitaji midogo na hivyo kuomba kupatia mikopo yenye riba nafuu ili kuwawezesha kuongeza kasi ya usambazaji wa pembejeo kwa wakulima .
Sanga alisema mikatati yake ni kuanza ufugaji wa ng’ombe kama 500 na kuku wa mayai kama 1500 ili kupitia mradi huo waweze kununua mazao ya wakulima kwa ajili ya mifugo .
Kwa upande wake Dkt Kikwete ameamepongeza jitahada kubwa zinazofanywa na AGRA nchini Tanzania katika kukuza kilimo na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo.
Dr Kikwete ambae aliweza kuwatembelea wachakataji wa mazao ya kilimo na wauzaji wa pembejeo na kujionea namna ambavyo wadau hao wa kilimo wamesaidia kujiongezea kipato na kutengeneza fursa nyingi za Ajira kwa wakulima wengi na hivyo kuwa kichocheo kikubwa cha ukuaji wa sekta ya Kilimo.
“Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Mipango ya AGRA,tulikubaliana kwenye Bodi kwamba wajumbe tupite kukagua miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa na AGRA.
Nimefarijika kuona miradi mingi ni mizuri na imeleta athari chanya kwa wakulima wetu na wachakataji wa mazao ya kilimo,hii itasaidia sana kukuza sekta ya kilimo na kukuza uchumi wa Nchi yetu”Alisema Dr Kikwete
Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde aliishukuru AGRA kwa kazi kubwa inayofanya katika kumjengea uwezo mkulima wa nchi hii na kuhakikisha kwamba zao la kilimo linaongezewa thamani jambo ambalo ndio muelekeo wa serikali na kuahidi kutoa ushirikiano kwa Taasisi hiyo ili malengo ya nchi kupitia kilimo yaweze kutimia.
Ziara hiyo mkoani Iringa Dr Kikwete aliambatana na makamu wa Rais wa AGRA Aggie Asimwe Konde pamoja na wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo.
0 Comments