Header Ads Widget

MGOMO WA MABASI IRINGA WATESA ABIRIA

 


MADEREVA   wa  mabasi  yanatoa  huduma  za  usafiri  katika mikoa  ya nyanda  za  juu  kusini Njombe , Mbeya  na Ruvuma  jana  wamegoma  kutoa  huduma   wakishinikiza  uongozi  wa  Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa kutengua zuio la mabasi hayo kuingia stendi  ndogo ya  Ipogolo .

Wakizungumza na  wanahabari   kuhusiana na  mgomo   huo  madereva  hao   walisema  wapo  tayari  kulipa  ushuru  wa  Halmashauri  mara  mbili  kwa maana  stendi  kuu ya mabasi ya  mikoani  iliyopo  Igumbilo  ambako  ni  mwanzo  wa  safari na watakapoingia  stendi ya  Ipogolo  kushusha ama  kupakia  abiria  pia  watalipa  ushuru .

Kwani  walisema  sababu  kubwa inayotajwa  na  uongozi wa Halmashauri ya  kutoruhusu  matumizi ya  stendi  hiyo ya  Ipogolo  ni  kukwepa  kuua  stendi ya  Igumbilo  ambayo  serikali imetumia  gharama  kubwa  katika  ujenzi  wa  stendi  hiyo jambo  ambalo wao  wapo  tayari  kuifanya  stendi  hiyo  kuendelea  kuingiza kipato cha Halmashauri kwa  kulipa ushuru kama kawaida.

Alisema  Obadia  Sanga  alisema  kuwa  hadi  sasa  wao  wamekuwa  wakitumia  stendi ya  Igumbilo  ambayo ni  stendi  ya  mkoa wa  Iringa  lakini daladala  za  Mafinga  zimekuwa  zikitumia  stendi  ya  Igumbilo na  stendi ya Ipogolo  jambo  ambalo  kwao  limekuwa  likiwatesa kwani  abiria  wao  wamekuwa  wakichukuliwa na daladala  za  Mafinga na kwenda  kuwafaulisha  Mafinga kwa  pesa  ambayo  ni  ndogo  kwao .

"  Tunachoomba   uongozi wa Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa  kuturuhusu tutumie  stendi ya  Ipogolo  kushusha  abiria  tunapotoka  Mbeya ama  Njombe na tunapokwenda mikoa hiyo  tukitokea  Igumbilo  basi  turuhusiwe  kuingia Ipogolo  kuchukua abiria  wa  mikoa ya  nyanda za  juu kusini " alisema 

Kwa  utaratibu wa sasa  si  tu  wanateseka  wao  wenye magari  bali ni utaratibu unaowatesa  hata  abiria  ambao  wanalazimika  kwenda  kushuka  Igumbilo  ndipo  waende Ipogolo ama  pindi  wanapotaka  kuondoka  basi  watumie  gharama  kubwa  kwenda  Igumbilo kutafuta  usafiri badala ya  kusubiri  usafiri  Ipogolo

Huku  Wamiliki  wa  mabasi hayo  walisema  kuwa   hawapo  tayari  kuingiza  mabasi yao  barabarani  kama   changamoto  hiyo haitapatiwa majibu ya  kueleweka maana  wanahisi  kuna  siasa ndani yake  alisema John Nyalusi .

Kuwa   wao kama  wamiliki  walishapeleka malalamiko yao kwa uongozi  wa Halmashauri  ya Manispaa ya  Iringa  kupitia mstahiki  meya ila  hawakujibiwa  kutokana na kukosa  muda wa  kukutana na meya kwa mazungumzo ya  changamoto hiyo.


Baadhi ya  wasafiri  waliokuwa  wakitegemea  usafiri  huo  kwenda mikoa ya  nyanda  za  juu  kusini  waliomba  uongozi  wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa na madereva  kumaliza  tofauti yao  kwani  wao abiria ndio  wanaoteseka kwa  mgomo  huo .

Anna Samson  alisema  kuwa alifika  stendi ya  Igumbilo  toka  saa 11 asubuhi  ili  kusafiri  kwenda  mkoani  Mbeya kwenye  mazishi lakini  hadi  saa 5 asubuhi  hakuweza  kusasfiri  zaidi ya  kusubiri mabasi ya Dodoma   ama  kutoka  Dar es salaam  ili  apande .


Hata  hivyo  madereva hao  ambao  walilazimika  kuendesha mabasi yao  bila  kupakia abiria  kutoka stendi ya Igumbilo zaidi ya  Kilomita 5  hadi stendi ya  Ipogolo kuegesha  kando  kando ya  barabara  kuu ya Iringa -  Mbeya  walizuiliwa na  jeshi la  polisi kuendelea  kuegesha mabasi yao  barabarani hapo kutokana na hali ya usalama  wao na  watumiaji  wengine wa barabara.

Mgomo  wa madereva hao  ni mwendelezo  wa  mgomo  ulioanza  wiki  mbili  zilizopita  ambapo mstahiki  meya  wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa  Ibrahim  Ngwada  alisema  kuwa  watakutana na madereva na wamiliki  hao  ili  kusikiliza kero yao na kuangalia jinsi gani ya  kuifanyia kazi .

Mkuu  wa  wilaya ya  Iringa Mohamed  Moyo  akizungumza kwa  njia ya  simu  kuhusiana na mgomo  huo  alisema  kuwa  stendi  inayotambuliwa ni  stendi ya  Igumbilo na sio  stendi ya  Ipogolo   hivyo mabasi yote ynayofanya  safari  zake  nje ya mkoa  wa Iringa yanapaswa  kutumia  stendi ya Igumbilo   na sio  Ipogolo.

















Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI